Jumatano, 11 Februari 2015

Innocent Melleck Shirima mwanaharakati wa vijana
Kijana Innocent Melleck Shirima awatahadharisha wananchi wa jimbo la vunjo kutokuja kufanya makosa ya mwaka 2010 kwa kumchagua mbunge ambaye leo hii ni mwiba mkali kama sio sindano inayowatesa katika mioyo yao katika uchaguzi mkuu ujao oktoba 2015 wa kuwapata viongozi wapya kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na uraisi.
Ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano maalumu na mtandao huu wa jamii.."nawasihi sana ndugu zangu wa vunjo kutorudia yale makosa ya mwaka 2010, kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa daraja zuri kati yao na serikali kuu, halmashauri, wafadhili wa ndani na nje na hata wananchi wenyewe kwa wenyewe na sio uwezo wake binafsi wa mali au utajiri"
Innocent Melleck Shirima anasema kuwa baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakiwaaminisha wananchi kuwa mbunge tajiri atawasaidia wananchi wake hata kama hana uwezo au maarifa ya kuwasaidia wananchi wake. Hali hiyo ndio ambayo imewapelekea wananachi wa jimbo la vunjo kukosa maendeleo kwa kipindi kirefu sana. Anasema kuwa mwaka 2010 kijana ambaye ndiye alipaswa kuwa mtu sahihi kuwawakilisha wananchi wa jimbo la vunjo (Crispin Meela) kutokana na uwezo wake wa kuwa daraja zuri kwao alikosa nafasi hiyo kwa imani tu hana uwezo wa kimali hatimaye wananchi wa jimbo la vunjo wakamchagua mbunge ambaye kwasasa kwao ni mwiba na hakuna anaetaka kumsikia.
Mkuu wa wilaya ya Rungwe Crispin Meela
Anaendelea kusema kuwa endapo wananchi wa jimbo la vunjo watarudia kosa la mwaka 2010 katika uchaguzi huu wa mwaka 2015 hakika watakuja kujutia sana kuliko hata namna ambavyo wanajutia hivi sasa. Anasema kuwa yupo mgombea kwa sasa amekuwa akiwalaghai wananchi wa jimbo la vunjo kwa kutumia pesa nyingi sana kwa kuzigawa huku akiwaaminisha kuwa ana uwezo mkubwa wa kuletea mabadiliko makubwa katika jimbo la vunjo.

James Mbatia mbunge wa kupitia Nccr-Mageuzi mwaka 1995
Amewataka wananchi kutokubali kudanganywa na hatimaye kurudia makosa tena. Anasema kuwa.."nawasihi sana hao wagombea kujipima kwanza kama wanafaa kuwawakilisha hao wananchi kwa kutizama rekodi zao za nyuma katika jimbo hilo la vunjo halafu ndipo wajitokeze mbele za wananchi. Kwani wananchi wa jimbo la vunjo bado wanakumbuka vizuri maumivu makali ya kimaisha waliyoyapata kipindi ambacho hao viongozi walipata hiyo fursa ya kuwawakilisha wananchi wa jimbo la vunjo"

Amewataka wananchi wa jimbo la vunjo kutokubali kudanganywa kuwa hao wanaotaka kupewa nafasi kwa mara nyingine kama wataweza kuwaletea maendeleo kama vile kuboresha vipato vyao kwa kuishawishi serikali kuwawekea mazingira bora kama vile kuwajengea miundombinu bora ya barabara, umeme pamoja na kunufaika na rasilimali mlima kilimanjaro. Anasema" kwanza wananchi wa vunjo wanapaswa kujiuliza haya maendeleo ambayo leo wanadai watakuja kuyaleta, kwanini kipindi walivyokuwa wabunge hawakuweza kutimiza hayo? iweje leo waje na kusema kuwa wataweza kuleta hayo mabadiliko? huo ni utapeli wa mchana kabisa"

Innocent Melleck Shirima
Anasema kwamba leo vijana wa jimbo la vunjo wanahangaika na namna ya kuboresha vipato vyao ili waweze kujiendesha na kujikimu maisha yao na familia zao lakini sote ni mashahidi juhudi ndogo ambazo zinazofanywa na hawa wawakilishi ambao wapo bungeni kukosa ushawishi kwa serikali kuu na hata wafadhili wa ndani na nje na hatimaye hali za vijana wa vunjo kuendelea kuwa katika wakati mgumu sana.

Anasema" nawaomba sana vijana waweze kuwahoji wabunge hao dhamira yao ya dhati kwao na sio tu dhamira yao iwe kuwatumia kisiasa kwa maslahi yao binafsi"

Mwisho, amewataka wananchi wa jimbo la vunjo kuwa wavumilivu kipindi hiki kigumu cha kuchagua viongozi wawatakao lakini wafanye maamuzi ya busara na sio ya kutaka kukomoa mtu au chama fulani.


0 maoni:

Chapisha Maoni

Inaendeshwa na Blogger.

Machapisho Maarufu

Machapisho ya Karibuni

Recent Posts Widget