Mtanzania Jitambue
facebook tweeter google linked in you tube rss
  • Home
  • Biashara
  • Burudani
    • Michezo
  • Siasa
  • Breaking News
    • Tanzania
      • Serikalini
  • Afya
  • Wazalendo
  • Ulimwenguni

KARIBU TANZANIA.

CLICK HERE FOR BREAKING NEWS.

BAADHI YA WAZALENDO KASKAZINI.

.

.

First slide Next

Alhamisi, 12 Februari 2015

  • 09:10
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO WAMUOMBA KADA WA CCM DAUD BABU MRINDOKO KUGOMBEA JIMBO LA MOSHI MJINI

Ndg. Daud Babu Mrindoko akiwa na baadhi ya akina mama wafanyabiashara ndogondogo
Katika tukio lisilokuwa la kawaida wakina mama ambao ni wafanyabiashara ndogondogo wamuomba kijana na kada wa chama cha Mapinduzi Ndg. Daudi Babu Mrindoko akubali wito wao wa kugombea jimbo la moshi mjini.
Tukio hilo limetokea mapema ya siku ya leo Alhamisi mara alipofika maeneo ya wafanyabiashara hao ili kupata mahitaji yake ya kawaida. Wakina mama hao ambao pia ni wafanyabiashara ndogondogo wamemtaka kijana huyo kugombea nafasi hiyo ya ubunge na kumuahidi kumuunga mkono katika kila hatua.
Wafanyabiashara hao wanasema kuwa wamelazimika kufanya hivyo hasa kutokana na kumfahamu vema kijana huyo uwezo wake wa kujitolea na kusaidia jamii. Baadhi yao wamesikika wakisema "kwasasa tunahitaji mabadiliko makubwa ya kiutawala mana hawa ambao wapo sasa bado hatujaona mchango wao kwetu, zaidi ni hali ya kimaisha kuzidi kuwa mbaya kila kukicha. Tunakuomba kijana wetu ukubali ombi letu mana tunatumbua uwezo wako wa kutumikia jamii"
Wafanyabiashara hao wamesikika wakisema safari hii hawatakubali kufanya makosa tena, shida ambayo wameipata kwa kipindi cha miaka kumi na tano hawapo tayari kuona hali hiyo inajirudia kwa mara nyingine tena..." Mwaka 2010 tulimpatia tena nafasi hiyo tukiamini kuwa kosa si kosa bali kurudia kosa, lakini bado makosa amezidi kuyarudia yale yale tena safari hii hali ndio mbaya zaidi sasa tumechoka na tunahitaji kufanya mabadiliko makubwa katika jimbo letu la moshi mjini"
Ndg. Daud Mrindoko akiwa anapata huduma
Kwa upande wa kijana huyo Ndg. Daudi Mrindoko amesema " Mimi kijana wenu sina mengi ya kuwaambia ila tuzidi ombeana kwa mwenyezi mungu mana ushauri wenu ni mzito sana, muda ukifika kila kitu kitakuwa wazi ila nimeupokea kwa mikono miwili ushauri wenu na hakika nitaufanyia kazi asanteni sana na mungu awabariki ninyi"
Wafanyabiashara wakiendelea na shughuli zao za kila siku sokoni
Read More
  • 08:04
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

MH. MREMA:-"MBATIA HANA UWEZO WA KUWA MBUNGE WA JIMBO LA VUNJO"

Mbunge wa jimbo la Vunjo Mh. Augustino L. Mrema akiwa katika kipindi maalumu cha mahojiano na redio Times fm ya jijini Dar es salaam juzi, amesema kwamba aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la vunjo mwaka 1995(James Mbatia) kwasasa hana uwezo wala jeuri ya kuwa mbunge wa jimbo la vunjo kwa mara nyingine tena.
Mbunge wa jimbo la vunjo Mh. Augustino Mrema
Aliyasema hayo kutokana na mchuano mkali uliopo jimboni kwake kwa baadhi wa watu mbalimbali kujitosa kutaka kupata ridhaa ya wananchi wa jimbo la vunjo kwa nafasi hiyo ya ubunge. Anasema kuwa Mh. James Mbatia hana nafasi kwa vunjo kwasababu tayari alishapewa nafasi kama hiyo mwaka 1995 tena mimi Mrema nikiwa mwenyekiti wake wa chama wakati huo, lakini sote ni mashahidi kwa kile ambacho amekifanya kipindi cha uongozi wake na mustakabali wa maisha ya jamii ya wanavunjo hali ilivyokuwa wakati huo.
Nikisema hafai si kwasababu namchukia la hasha ila uwezo wake wa kuwatumikia wananchi na rekodi yake ndio inayomhukumu moja kwa moja. Anasema kuwa kwa kipindi cha miaka mitano aliyowahi kuwa madarakani hakuna jipya la maana alilowahi kulifanya katika mambo ya elimu, barabara, umeme, kilimo, maji, afya, mazingira, ulinzi na usalama, michezo pamoja na uboreshaji wa kipato cha mtu mmoja mmoja sasa leo akisema anaouwezo wa kuyafanya hayo huo ni uongo uliokithiri na kuwafanya wananchi wa jimbo la vunjo ni wajinga kupita kiasi huku ni sawa na kuwadharau.
Mrema II
Mh. James Mbatia akiwa na Mh. Mrema
Wakati huo huo, katika hali isiyo ya kawaida mbunge huyo wa vunjo mh. Mrema amesema kwasasa mtu ambaye ana uwezo mkubwa kama akikosa nafasi ya kuwawakilisha wananchi wa vunjo bungeni katika uchaguzi wa oktoba 2015 ni mmoja tu kwa wote ambao tayari wamejitokeza nae si mwingine bali ni kijana INNOCENT MELLECK SHIRIMA.
Anasema akimzungumzia kijana huyo ni kwamba ni mtu pekee na sahihi kwa watu wa jimbo la vunjo hasa kutokana na uwezo na kipaji chake alichonacho cha kuwatumikia wananchi. Anasema kuwa huyu ni kijana ambaye wananchi wa jimbo la vunjo wanapaswa kutokuja kufanya makosa hata kidogo na wahahakishe wanamchagua ili aweze kuwatumikia ipasavyo.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhqDOtlc68k4RfZS4HXD6QSvWIk6ZXhr_hE68KNoEi12GVfUX3DfKoAoNbsFG477kUsU9fE0hyphenhyphenCpu4XDUy2JzIGIwM7ervHpWsz2BUlRVzRtuwULkGfIKuK833r-GRJZAxHZdZn9sWp-CI/s1600/unnamedI1.jpg
Innocent Melleck
Anasema.." Mtu sahihi kwa vunjo kama sio mimi mrema basi ni yule kija Innocent Melleck na sio wengine, hivyo wananchi wangu wa jimbo la vunjo msikubali kununulika hata kidogo"
Pia, ametumia muda huo kukanusha tuhuma zote zilizoelekezwa kwake na Mh. James Mbatia dhidi yake, amemtaka kufanya siasa safi na sio hizo anazoendelea nazo kwasasa hivi kwasababu hazijengi bali hubomoa.
Read More

Jumatano, 11 Februari 2015

  • 08:22
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

KIJANA INNOCENT MELLECK SHIRIMA AWATAHADHARISHA WANAVUNJO KUTORUDIA MAKOSA YA 1995, 2000 NA 2010

Innocent Melleck Shirima mwanaharakati wa vijana
Kijana Innocent Melleck Shirima awatahadharisha wananchi wa jimbo la vunjo kutokuja kufanya makosa ya mwaka 2010 kwa kumchagua mbunge ambaye leo hii ni mwiba mkali kama sio sindano inayowatesa katika mioyo yao katika uchaguzi mkuu ujao oktoba 2015 wa kuwapata viongozi wapya kuanzia ngazi ya udiwani, ubunge na uraisi.
Ameyasema hayo alipokuwa akifanya mahojiano maalumu na mtandao huu wa jamii.."nawasihi sana ndugu zangu wa vunjo kutorudia yale makosa ya mwaka 2010, kiongozi mzuri ni yule ambaye atakuwa daraja zuri kati yao na serikali kuu, halmashauri, wafadhili wa ndani na nje na hata wananchi wenyewe kwa wenyewe na sio uwezo wake binafsi wa mali au utajiri"
Innocent Melleck Shirima anasema kuwa baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakiwaaminisha wananchi kuwa mbunge tajiri atawasaidia wananchi wake hata kama hana uwezo au maarifa ya kuwasaidia wananchi wake. Hali hiyo ndio ambayo imewapelekea wananachi wa jimbo la vunjo kukosa maendeleo kwa kipindi kirefu sana. Anasema kuwa mwaka 2010 kijana ambaye ndiye alipaswa kuwa mtu sahihi kuwawakilisha wananchi wa jimbo la vunjo (Crispin Meela) kutokana na uwezo wake wa kuwa daraja zuri kwao alikosa nafasi hiyo kwa imani tu hana uwezo wa kimali hatimaye wananchi wa jimbo la vunjo wakamchagua mbunge ambaye kwasasa kwao ni mwiba na hakuna anaetaka kumsikia.
Mkuu wa wilaya ya Rungwe Crispin Meela
Anaendelea kusema kuwa endapo wananchi wa jimbo la vunjo watarudia kosa la mwaka 2010 katika uchaguzi huu wa mwaka 2015 hakika watakuja kujutia sana kuliko hata namna ambavyo wanajutia hivi sasa. Anasema kuwa yupo mgombea kwa sasa amekuwa akiwalaghai wananchi wa jimbo la vunjo kwa kutumia pesa nyingi sana kwa kuzigawa huku akiwaaminisha kuwa ana uwezo mkubwa wa kuletea mabadiliko makubwa katika jimbo la vunjo.

James Mbatia mbunge wa kupitia Nccr-Mageuzi mwaka 1995
Amewataka wananchi kutokubali kudanganywa na hatimaye kurudia makosa tena. Anasema kuwa.."nawasihi sana hao wagombea kujipima kwanza kama wanafaa kuwawakilisha hao wananchi kwa kutizama rekodi zao za nyuma katika jimbo hilo la vunjo halafu ndipo wajitokeze mbele za wananchi. Kwani wananchi wa jimbo la vunjo bado wanakumbuka vizuri maumivu makali ya kimaisha waliyoyapata kipindi ambacho hao viongozi walipata hiyo fursa ya kuwawakilisha wananchi wa jimbo la vunjo"

Amewataka wananchi wa jimbo la vunjo kutokubali kudanganywa kuwa hao wanaotaka kupewa nafasi kwa mara nyingine kama wataweza kuwaletea maendeleo kama vile kuboresha vipato vyao kwa kuishawishi serikali kuwawekea mazingira bora kama vile kuwajengea miundombinu bora ya barabara, umeme pamoja na kunufaika na rasilimali mlima kilimanjaro. Anasema" kwanza wananchi wa vunjo wanapaswa kujiuliza haya maendeleo ambayo leo wanadai watakuja kuyaleta, kwanini kipindi walivyokuwa wabunge hawakuweza kutimiza hayo? iweje leo waje na kusema kuwa wataweza kuleta hayo mabadiliko? huo ni utapeli wa mchana kabisa"

Innocent Melleck Shirima
Anasema kwamba leo vijana wa jimbo la vunjo wanahangaika na namna ya kuboresha vipato vyao ili waweze kujiendesha na kujikimu maisha yao na familia zao lakini sote ni mashahidi juhudi ndogo ambazo zinazofanywa na hawa wawakilishi ambao wapo bungeni kukosa ushawishi kwa serikali kuu na hata wafadhili wa ndani na nje na hatimaye hali za vijana wa vunjo kuendelea kuwa katika wakati mgumu sana.

Anasema" nawaomba sana vijana waweze kuwahoji wabunge hao dhamira yao ya dhati kwao na sio tu dhamira yao iwe kuwatumia kisiasa kwa maslahi yao binafsi"

Mwisho, amewataka wananchi wa jimbo la vunjo kuwa wavumilivu kipindi hiki kigumu cha kuchagua viongozi wawatakao lakini wafanye maamuzi ya busara na sio ya kutaka kukomoa mtu au chama fulani.


Read More

Jumanne, 10 Februari 2015

  • 11:54
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

UN YAIPA LAWAMA TANZANIA KWA HALI ILIVYO DRC


Hali ilivyo DRC
Umoja wa mataifa imezituhumu serikali za Tanzania na Burundi kuhusiana na hali katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Ripoti
mpya ya kundi la wataalamu wa umoja huo kuhusu Congo, imeituhumu
Tanzania kwa kuwaruhusu viongozi wa kundi la waasi wa FDLR kuandaa
mikutano nchini humo.

Imeeleza pia kwamba wanajeshi wa Burundi wametekeleza unyanyasaji wa kingono.

Taarifa
hiyo ya Umoja wa mataifa inasema kuwa tangu mwaka wa 2013, viongozi wa
FDLR na baadhi ya washirika wao wa kisiasa kutoka Ulaya wamekuwa
wakikutana nchini Tanzania.

Majeshi ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo wakipambana na waasi
Lakini wachunguzi wa Umoja wa
mataifa walipoiuliza serikali ya Tanzania kujibu madai haya ilikanusha
kabisa kuwahi kuakaribisha mikutano yoyote ya waasi ndani ya ardhi yake
na kuongeza kuwa hakujawahi kuwa na mazungumzo yoyote kati ya majeshi
yake na wapiganaji wa FDLR.

Umoja wamataifa umesema pia kuwa una
ushahidi wa pesa zilizotumwa kutoka taifa hilo la Afrika Mashariki kwa
baadhi ya washukiwa nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Ripoti
hiyo pia imelaumu kundi hilo la FDLR kwa kutotekeleza ahadi yao ya
kusalimisha silaha na kujisalimisha kufikia Januari mwaka huu.

UN
inasema kuwa FDLR wamewatuma wazee waliodhoofika kiafya pekee
kujisalimisha na kukabidhi silaha chache sana ambazo zina hitilafu.

Kundi
la FDLR, liliundwa mwaka wa 2000 na wahutu waliokimbilia Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo kufuatia mauaji ya kimbari ya Rwanda.

Wapiganaji wa kundi la FDLR
Kundi hilo linapinga utawala wa kitutsi na ushawishi wake katika eneo la maziwa makuu.

Rwanda
imekuwa ikitazama kundi hilo kama tisho kubwa kwa utawala uliopo na kwa
kauli moja na Umoja wa mataifa imekuwa ikishinikiza kupokonywa silaha
kwa wapiganaji wake.

Ripoti hiyo pia imetoa madai ya ubakaji na unyanyasaji wa kimapenzi unaofanywa na wanajeshi wa Burundi katika Kivu ya Kusini .

Wataalamu
hao wa Umoja wa mataifa wamependekeza serikali za Burundi na Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo zifanyie uchunguzi madai hayo ambayo wanasisitiza
yalifanywa namajeshiya Burundi pamoja na kikundi cha vijana wapiganaji
wajulikanao kama Imbonerakure.



@bbc news


Read More
  • 07:05
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

MHESHIMIWA Rais Prof.JAKAYA KIKWETE AFUNGUA RASMI LEO JENGO LA NSSF MOSHI-KILIMANJARO

Mheshimiwa Rais.Prof.Jakaya Kikwete afungua Jengo la NSSF-KILIMANJARO
NSSF yajenga jengo kubwa sana Mjini Moshi, Mhe.Rais Kikwete amewapongeza sana Mhe.Kabaka-Waziri wa Ajira na Kazi pamoja Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro Mhe.Gama pia walikuwepo Mhe.Mrima-Mbunge wa Vunjo pamoja na Mhe.Chami-Mbunge wa Moshi Vijijin pamoja viongozi wa Vyama vyote akiwemo Mwenyekiti wa CCM MKOA-Ndg.Idd Mwanaweza..
Rais  Jakaya aliwapongeza sana wabia wate walioshirikiana na NSSF kutoa maeneo yenu na kujengwa Jengo..
Napenda kuwapongeza sana tena sana Uongozi wa NSSF-Ndg.Ramadhani Dau hongereni sana..Pia mmeweza kufanya jambo zuri ambalo litakuwa mnapata Mikutano pia nimeambiwa kuna Hotel/Ofisi/Sehemu za Biashara kwa hiyo tushukuru kipata kitaongezeka na ajira zitaongezeka pia na kipato kitaongezeka pia, Manspaa ya Moshi mtabidi mpokee maombi ya NSSF ili muweze kuongea vizuri kuweza kupata parking,
Pia TAASISI nyingine nawaombeni mutenge sehemu ya kujenga magorofa, Uwe Meya wa maendeleo siyo Meya wa Mbwembwee tu sasa watu wanataka maeneo ya Kujenga..
Hata kesho picha zikatoka kesho basi wawekezaji watakuja kuwekeza ila Manspaa mkitaka kutanuka ni kutanunikia Moshi Vijijini ila Moshi Vijijini ni Kazi kwani wanapenda Viwamba, Nakumbuka siku moja nikiwa ofisi ya Chama nikiwa makao makuu nilikuwa naratibu wageni kumuona Hayati Mwl.Nyerere:Alikuja Mzee Mmoja hivi akatoa vikambakamba hivi kama Saba (7) hivi na akaniuliza unavijua hivi mwanangu nikasema:Sijui yeye akasema kwenye Eneo hili watoto nimewazalia hapo itakuwaje iwe mjini tena!!
Nashukuru sana kwa wana Moshi na ntakuja kwa ajili ya Ziara ya Serikali kipindi kijacho! Ahsanteni sanaaa
Mwenyekiti wa Bodi ya NSSF amshukuru Rais Prof.Kikwete kwa kuja kufungua Jengo na kuwapa moyo ya kuweza na pia Nasema ILANI YA CCM inatekeleza hata kama hawataki ila wanatekeleza na naomba CCM, Na Tutahakikisha CCM inashinda tena na kuendelea kuwa madakani.Ahsante sana Karibu Mhe.Prof.Kikwete

Wenu MTANZANIA JITAMBUE-MOSHI KILIMANJARO...

Read More

Jumapili, 8 Februari 2015

  • 01:32
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

INNOCENT MELLECK SHIRIMA KIJANA ALIYEPANIA KURUDISHA HESHIMA YA JIMBO LA VUNJO

Innocent Melleck Shirima akihutubia mamia ya wanavunjo

Innocent Melleck ni kijana mzaliwa Marangu wilayani moshi vijijini mkoani Kilimanjaro lakini pia ni naibu kamanda wa vijana wilaya ya moshi vijijini kupitia UVCCM.
Kwa kipindi kirefu sana kijana huyu amekuwa katika hali ya kutoridhishwa na maendeleo ya jimbo la vunjo, hali ambayo imemlazimu kufanya jitihada za kuweza kusaidiana na wananchi wa jimbo la vunjo kuhakikisha wanaenda kasi ya kuwaletea maendeleo wanavunjo kwa ujumla wao.
Kijana huyo anaamini kuwa kasi ya maendeleo ya vunjo haiendani na uhalisia wa rasilimali ambazo zipo au zilizozunguka eneo hilo. Amenukuliwa akisema" Tukitazama uhalisia wa maendeleo ya jimbo la vunjo na rasilimali ambazo zipo haziwiani hata kidogo. Tuna rasilimali nyingi na za kipekee kabisa kwa mfano huu mlima kilimanjaro na rasilimali ardhi tuliyonayo hivi kunasababu gani ya maendeleo kutoenda kwa kasi kiasi cha kuridhisha?"
Mount Kilimanjaro
Mlima Kilimanjaro

Innocent Melleck anasema rasilimali hizi zinatosha kwa kiasi kikubwa sana kuifanya vunjo kuwa na maendeleo makubwa sana bila utegemezi wa serikali kuu. Kupitia mlima huu kuna uwekezaji mkubwa sana ambao haumfaidishi moja kwa moja mkazi wa eneo husika bali ni serikali kuu ambayo mahitaji kiasi kikubwa hupelekwa maeneo mengine ambayo kwa namna moja ama nyingine wawakilishi wao wana nguvu ya kujenga hoja na ushawishi bungeni.
Watalii wakipanda Mlima kilimanjaro
Kijana huyu anasema kuwa vunjo inapaswa kuwa mahala kwa mfano wa kuigwa mahala pengine hasa kwa kuweza kunufaika na rasilimali hizo muhimu ardhi na mlima kilimanjaro lakini hali iko tofauti sana na ilivyotarajiwa. Anasema kuwa" Ni aibu sana kwa jamii ya wanavunjo kulalamika kuwa kuna tatizo la barabara, maji, umeme, hospitali na zahanati pamoja na pembejeo za wakulima. Milima wa kilimanjaro unaingiza mapato kwa kiasi kikubwa sana. Sote ni mashahidi ni kwa kiasi gani watalii wanavyomiminika kuja kutizama na kuupanda mlima huu wa kilimanjaro, leo kuwa na changamoto za aina hii ndio jambo ambalo limenisukuma sana kuangalia kwa namna gani kuweza kubadili mfumo mzima wa uwakilishi wa eneo letu la vunjo pamoja kuhakikisha tunaleta maendeleo kwa kasi inayoridhisha"
Ramani ya Mlima Kilimanjaro

Innocent Melleck ameawataka wanavunjo wasikate tamaa kupigania maslahi yao lakini kwanza ni lazima kuhakikisha kuwa wanafanya mabadiliko ya uwakilishi wao, mana kichooneka hapa ni suala la uwakilishi ndio tatizo. Tusikubali kurudia makosa ambayo yalitugharimu sana mwaka 1995-2000 awamu ya aliyekuwa mbunge kipindi hicho MBATIA, 2000-2005 na 2010-2015 makosa haya ndiyo ambayo yametufanya leo hii tunazungumza mengi kuhusu vunjo yetu kwanini kasi ya maendeleo ipo chini kiasi cha kuhatarisha maisha ya vijana wengi kwa kukosa ajira na wazee kukosa malezi toka kwa vijana wao ambao ndio nguvu kazi wanayoitegemea.
Mabadiliko kufanyika si jambo la kushauriana wala la kusita, hili ni jambo la ulazima kuliko mambo mengine yoyote yale. Jambo hili linahitaji muda na maamuzi sahih. Mwaka huu ni kipindi cha uchgauzi mkuu wa serikali kwa ngazi ya udiwani, ubunge na Uraisi ni kipindi ambacho wanavunjo wanapaswa kufanya maamuzi ambayo hawatakuja kuyajutia kwa kipindi kingine cha miaka mitano ijayo.
Innocent Melleck amewataka wanavunjo wote bila kujali itakidai zao kumchagua kiongozi ambaye atakuwa na uwezo wa kushawishi serikali kuu kwa hoja ili aweze kuwaletea maendeleo ya kasi katika jimbo la vunjo.
Anaendelea kusema kuwa ni kweli watakuja wengi sana na vyama vyao kuomba ridhaa kwenu, lakini pia wapo ambao watakuja kwenu bila kuona haya kwa kujiuliza kipindi ambacho walipewa ridhaa na sisi wanavunjo waliitumika vipi na kwanini hali ni mbaya na sasa wana mbinu gani mpya ya kuwasaidia wanavunjo ili waweze kuwaamini kwa mara nyingine. Watu wa aina hiyo tuwaogope kama ugonjwa wa ukoma.
Kwa upande wake ameweka dhamira ya kweli kuja kufanya mapinduzi makubwa sana ya kimaendeleo na ana imani wanavunjo kwa umoja wao watamuunga mkono katika harakati hizo. Na ameamua kufanya hivyo baada ya maombi mengi toka kwa vijana na wazee wa jimbo la vunjo lakini pia amefarijika kuona wapo tayari kumchukulia fomu za kuomba ridhaa kwa gharama zao wenyewe.

Mwisho amewataka wanasiasa wote ambao wanadhamira ya kutaka kuomba ridhaa kwa wanavunjo kuweza kujiuliza mara mbili kama anatosha au la, lakini pia wamuogope mungu kwa matendo yao dhidi ya wananchi wa vunjo.




Read More

Jumamosi, 7 Februari 2015

  • 00:37
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

PICHA ZA MATUKIO ZA MH. OLIVIA SANARE ALIPOHUDHURIA MAAZIMISHO YA MIAKA 38 YA CCM MKOANI RUVUMA

Kada wa ccm Olivia Sanare akiwa na baadhi ya walioshiriki maadhimisho uwanjani 
Picha ya kwa pamoja na mh. Olivia Sanare

Mh. Olivia Sanare
Olivia Sanare akifurahia jambo

Read More
  • 00:20
  • Mtanzania Jitambue
  • No comments

WAASI WA HOUTH WACHUKUA SERIKALI NCHINI YEMENI

                                  

Waasi wa Shia wametangaza kutwaa
uongozi wa kisiasa nchini Yemen, kuvunjilia mbali bunge, kumwondoa rais
na nafasi hiyo kuchukuliwa na baraza la urais.
Wahouthi hao
walitangaza hayo katika mkutano wa siasa walipokuwa na jeshi na wakuu wa
makabila katika ikulu ya nchi katika mji mkuu, Sanaa.



Waasi wa houth
Tukio hilo linajiri baada ya mazungumzo yaliyoongozwa na umoja wa mataifa ya kukomesha mzozo wa Yemen kusambaratika.

Rais Mansour Abdrabbuh Hadi na serikali yake walijiuzulu mwezi uliopita baada ya waasi hao kuthibiti mji wa Sanaa.
Read More

Jumatatu, 2 Februari 2015

  • 13:55
  • Mtanzania Jitambue
  • Siasa, UVCCM
  • 1 comment

UVCCM MOSHI VIJIJINI WATIA FORA MIAKA 38 YA CCM

Mjumbe wa mkutano mkuu ccm taifa na mwenyekiti wa kamati ya uchumi uvccm mkoa wa kilimanjaro Ndg. Jerome Komu akikagua timu za mpira uwanjani
Mgeni rasmi akifatilia mpambano kwa ukaribu sana
Mgeni rasmi akikabidhi zawadi kwa washindi wa mechi ya fainali
Picha ya kwa pamoja na washindi
Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano wa hadhara
 Vijana wakifurahia zawadi zao za ushindi
Mgeni rasmi akihutubia mkutano wahadhara wa kijiji cha Mtakuja

Mwenyekiti wa kijiji cha chekereni akihutubia wananchi

Katibu hamasa uvccm moshi vijijini Ndg. Hassan husein akihutubia mkutano wahadhara

Katibu wa uvccm moshi vijijini akijiandaa kuhutubia mkutano wa hadhara

Mgeni rasmi akipokea wanachama wapya wa uvccm kijiji cha chekereni






Read More
  • 08:42
  • Mtanzania Jitambue
  • Siasa
  • No comments

CCM WILAYA YA MOSHI VIJIJINI YAADHIMISHA MIAKA 38 YA KUZALIWA KWAKE KWA KUWATEMBELEA WAGONJWA HOSPITALI YA KILEMA MKOANI KILIMANJARO

Viongozi wa chama cha mapinduzi wilaya ya moshi vijijini wakiwasili hospitali ya Kilema
Chama cha Mapinduzi wilayani moshi vijijini siku ya Jumapili tarehe 01/02/2015 kimeadhimisha miaka 38 kuzaliwa kwake kwa kutembelea wagonjwa waliolazwa hospitali ya Kilema. Wakiongozwa na Katibu wa wilaya wa chama hicho Ndg. Mirism S. Kaaya waliweza kutoa misaada mbalimbali kwa wagonjwa hao waliwakuta hospitalini hapo.



Katibu wa CCM wilaya ya Moshi vijijini Miriam S. Kaaya akisaini daftari la wageni mara alipowasili hospitalini hapo
Baadhi ya misaada waliyotoa hospitalini hapo ni pamoja na vyakula, sabuni za kufulia na kuogea, dawa za miswaki n.k. Zawadi hizo zimetolewa kwa lengo la kuwafariji na kuwaombea kwa mungu wapone kwa haraka ili waweze kurejea katika hali zao za kawaida



Katibu wa itikadi na uenezi CCM wilaya ya Moshi vijijini Ndg. Husein Jamal akisaini kitabu cha wageni hospitalini hapo
Huu ni utaratibu wa kawaida wa chama hicho kufanya kazi za kijamii mara kwa mara. Akihojiwa Katibu wa wilaya wa CCM moshi vijijini Miriam Kaaya amesema "Hili ni jambao la kawaida kwa chama cha mapinduzi kufanya shughuli za kijamii, tunaazimisha miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM kama ofisi ya wilaya safari hii imeona iadhimishe kwa aina hii ya kuwatembelea wagonjwa wa hospital ya Kilema"



Katibu wa CCM wilaya akimfariji mgonjwa ambaye kwa sasa yupo kitandani kwa muda wa mwaka mzima hospitalini hapo
Pia, katibu wa CCM wilaya moshi vijijini ametumia nafasi hiyo kuwapa pole wagonjwa na kuwaombea wapone haraka ili waje kujena Taifa lao. Akinukuliwa akisema " Tumekuja kuwatembelea ili kuwapa pole kwa kuumwa lakini pia kuzidi kuwaombea kwa mungu mpone kwa haraka ili mrudi kulitumikia taifa lenu"



Katibu wa itikadi na uenezi CCM wilaya moshi vijijini Ndg. Husein Jamal akimfariji mtoto aliyevunjika mguu alipotembela wodi ya wagonjwa hiyo
Viongozi wengine waliombata katika msafara huo ni makatibu wa jumuiya za chama hicho Ndg. Kulwa(Katibu msaidizi CCM wilaya), Ndg. Abdulkarim Halamga(Katibu Uvccm wilaya), Ndg. Justina Bayo(Katibu Uwt wilaya), Ndg. Hassan husein(Katibu Hamasa Uvccm wilaya) na viongozi mbali mbali wa Kata ya Kilema Kusini.



Katibu wa Uvccm wilaya moshi vijijini Ndg. Abdulkarim Halamga akikabidhi msaada kwa mgonjwa wodi ya wazazi
Ujio huo umewapa matumaini makubwa wagonjwa wa hospitalini hapo. Wagonjwa wameshukuru kwa kitendo hichokilichofanywa na chama cha mapinduzi wilaya ya moshi vijijini na kuvitaka vyama vingine kuiga mfano wa chama hicho kikongwe nchini.



Katibu wa CCM wilaya akiwa amembeba mtoto mchanga wodi ya wazazi


 FUATILIA PICHA ZA MATUKIO

Katibu Hamasa Uvccm wilaya ya moshi vijijini Ndg. Hassan husein akikabidhi zawadi mbalimbali kwa wagonjwa
Katibu wa UWT wilaya ya moshi vijijini Ndg. Justina Bayo akiwa amembeba mtoto mchanga
Picha ya kwa pamoja viongozi wa chama cha mapinduzi na viongozi wa hospitali ya Kilema


















Read More
← Machapisho Mapya Machapisho ya Zamani → Nyumbani
Jisajili kwenye: Maoni (Atom)

Lebo

  • Biashara
  • Michezo
  • Serikalini
  • Siasa
  • Tanzania
  • Ulimwenguni
  • UVCCM
  • Wazalendo

Kumbukumbu la Blogu

  • ►  2024 (2)
    • ►  Julai (2)
  • ▼  2015 (22)
    • ►  Septemba (1)
    • ►  Aprili (2)
    • ►  Machi (5)
    • ▼  Februari (10)
      • WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO WAMUOMBA KADA WA CCM D...
      • MH. MREMA:-"MBATIA HANA UWEZO WA KUWA MBUNGE WA JI...
      • KIJANA INNOCENT MELLECK SHIRIMA AWATAHADHARISHA WA...
      • UN YAIPA LAWAMA TANZANIA KWA HALI ILIVYO DRC
      • MHESHIMIWA Rais Prof.JAKAYA KIKWETE AFUNGUA RASMI ...
      • INNOCENT MELLECK SHIRIMA KIJANA ALIYEPANIA KURUDIS...
      • PICHA ZA MATUKIO ZA MH. OLIVIA SANARE ALIPOHUDHURI...
      • WAASI WA HOUTH WACHUKUA SERIKALI NCHINI YEMENI
      • UVCCM MOSHI VIJIJINI WATIA FORA MIAKA 38 YA CCM
      • CCM WILAYA YA MOSHI VIJIJINI YAADHIMISHA MIAKA 38 ...
    • ►  Januari (4)
  • ►  2014 (97)
    • ►  Desemba (34)
    • ►  Novemba (27)
    • ►  Oktoba (3)
    • ►  Septemba (33)
Inaendeshwa na Blogger.

Machapisho Maarufu

  • WANANCHI WA MJI MDOGO WA HIMO WAJITOKEZA KWA WINGI KUSHANGILIA USHINDI WA CCM
    Siku ya jana tarehe 21/12/2014 wakazi wa mji mdogo wa Himo wajitokeza kwa wingi sana kusherehekea ushindi wa kishindo wa chama cha mapinduzi...
  • break News:MABUS YA KILENGA YAGONGANA ILA YAMEARIBIKA KIDOGO.
    Ajali imetokea hapa daraja la kifaru Himekuwa ya Ajabu ajabu ni Bus moja la Kilenga limegonga nyuma ya Gari lingine la Kilenga majira ya 10...
  • PICHA ZA MATUKIO ZA MH. OLIVIA SANARE ALIPOHUDHURIA MAAZIMISHO YA MIAKA 38 YA CCM MKOANI RUVUMA
    Kada wa ccm Olivia Sanare akiwa na baadhi ya walioshiriki maadhimisho uwanjani   Picha ya kwa pamoja na mh. Olivia Sanare Mh. Oliv...
  • CHIEF MRINDOKO: "MUDA UKIFIKA NITAJIBU MAOMBI YENU YA KUNISHAWISHI KUGOMBEA UBUNGE MOSHI MJINI"
    Leo Jumapili tarehe 12/04/2015, mwenyekiti wa taasisi ya wazalendo Taifa Ndg. Chief Daud Mrindoko ameyasema hayo katika uzinduzi wa Album ya...
  • MWENYEKITI UVCCM MKOA WA KILIMANJARO AZINDUA RASMI UVCCM CUP KATA YA MAKUYUNI
    Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Kilimanjaro Ndg. Fredrick Mushi akihutubia mashabiki wa soka waliohudhuria uzinduzi huo wa ligi ya UVCCM CUP kat...
  • CCM WILAYA YA MOSHI VIJIJINI YAADHIMISHA MIAKA 38 YA KUZALIWA KWAKE KWA KUWATEMBELEA WAGONJWA HOSPITALI YA KILEMA MKOANI KILIMANJARO
    Viongozi wa chama cha mapinduzi wilaya ya moshi vijijini wakiwasili hospitali ya Kilema Chama cha Mapinduzi wilayani moshi vijijin...
  • MASANJA AKUTANA YESU !!!
    Ni mfabiashara maarufu mjn moshi anaitwa Yesus pafyum au Sharif Mussa msanii maarufu na mchungaji ndg Emanuely Mgaya almaarufu Masanja mkan...
  • KADA WA CCM NDG. OLIVER SANARE ASHIRIKI HARAMBEE NA UZINDUZI WA KWAYA KATIKA KANISA LA MAWELA URU WILAYA YA MOSHI VIJIJINI
    Ndg. Oliver Sanare akisema jambo katika harambee ya kanisa la Mawella  Kada wa chama cha Mapinduzi Ndg. Oliver Sanare siku ya jana tar...
  • BREAKING NEWS: HELCOPTER YAPATA AJALI NA KUUA WATU WANNE MAENEO YA MOSHI BAR- UKONGA LEO MAPEMA
    Mabaki ya helcopter iliyoanguka maeneo ya Moshi bar- Ukonga wilayani Ilala Helcopter mali ya serikali wizara ya mali asili yaa...
  • DR.SLAA AFUNGUKA UKWELI...UKAWA MASHAKANI
    LIVE UPDATE Kutoka Serena Hotel Ambako Dr. Slaa Anaongea 1.Napenda  kumshukuru  mwenyezi  mungu  kwa  kutujali  uzima. 2. Nimeamua  kujito...

Machapisho ya Karibuni

Recent Posts Widget

Kurasa

  • Home

Kunihusu

Mtanzania Jitambue
Tazama wasifu wangu kamili

Sample Text

Copyright © Mtanzania Jitambue | Powered by Blogger
Template Designed by Kanoutechno™
Blogger Templates