(Mb) James Mbatia
Mbunge wa kuteuliwa na Rais (Mb) James Mbatia ameiambia radio KILI FM 87.5 Mhz ya Moshi Mkoani kilimanjaro wakati wa mahojiano yake tarehe 20/02/2015 siku ya Ijumaa kuwa kipindi alipokua mbunge wa jimbo hilo 1995 mpaka 2000 alishindwa kufanya vema upande wa michezo kwasababu wananchi wa vunjo hawapendi michezo hiyo bali wao hupenda zaidi pombe(VITOCHI).
Hayo yalitokana na swali aliloulizwa na mtangazaji wa kipindi hicho juu suala la maendeleo ya michezo kuwa nyuma sana katika jimbo la vunjo. (Mb) James Mbatia alisema"Swali lako ni zuri sana ndugu mtangazaji, nakumbuka kipindi ni mbunge nilijaribu kukuza michezo lakini wazee wakanionya kuwa hawataki, wao wanahitaji vitochi"
Pia, alitoa msimamo wake wa kutozikubali hata kidogo shule za kata za serikali ijapokuwa amewahi kuzitembelea shule hizo.
0 maoni:
Chapisha Maoni