Jumatatu, 30 Machi 2015

Mabalozi wa Usalama Barabarani wafanya Kikao Kujadili Suala la Ajali nchini. Na Kupata Semina Ya Bima kwa Mtaalam Bw. Mwandu

Shukrani

 KWA RSA WOTE.

Kwa namna ya pekee kabisa na moyo wa dhati natumia fursa hii kuwashukuru RSA wote ambao mmejitoa kwa moyo mmoja kuhudhuria mkutano wa leo war obo mwaka uliofanyika Police Officers’Mess Jijini Dar es Salaam. Kwa kweli, japo sikuwepo nanyi, lakini nimehamasika sana, kila nilipoona picha zenu na kusikia sauti zenu toka kwenye recordings mlizokuwa mkizituma niliona nimekosa kitu kikubwa sana. Mahudhurio yenu yamenifanya nijiulize maswali mengi sana, kuwa wakati nimejikuta nikitokwa na machozi, lakini tofauti na machozi mengine haya yalikuwa machozi ya furaha.Binafsi kama moja ya waanzilishi wakubwa wa mtandao wa RSA nimefarijika sana kuona kwamba kumbe kitu tulichokianzisha kama utani vile sasa kimeshika kasi na kukita mizizi mioyoni mwa watu kiasi kwamba kinakuwa cha kitaifa. Pale unaposikia watu wametoka Mwanza, Arusha, Mbeya, Songea nk kwaajili ya kuja kuhudhuria mkutano wa RSA tu then inakubidi utafakari mara mbili tatu commitment watu waliyonayo katika kuhakikisha kuwa kuna usalama barabarani. Kila mmoja wetu naomba atafakari hili na mkutano wa leo uwe chachu mpya ya kuongeza mashambulizi dhidi ya ajali. Unapoona watu na vyeo vyao tena vikubwa kabisa kama vile Wakurugenzi wa mashirika mbalimbali ya umma na binafsi, watendaji wakuu, askari wav yeo vya juu kabisa, watu wazima kwa umri nk wanajiunga na rsa na wanakubali kukaa kwenye mkutano kuanzia saa 8 mchana hadi saa 2 Usiku hapo ndipo utakapoona umuhimu wa hili jambo.Hawa watu sio kwamba hawana kazi za kufanya, je ni nini kina waleta rsa? Wala hatugawi hela, wala rsa hakuna posho, wala hakuna vyeo vya kisiasa lakini watu hawaachi kuja. Nimeguswa Zaidi na rsa wenzetu ambao pamoja na kupata msiba leo hii bado waliweza kufika, na kuna rsa mwenzetu pamoja na kuwa na msiba huko Iringa wiki hii bado aliweza kupanda ndege na kufika Dar ili kuwahi mkutano. Kuna watu wamekodi vyombo mbalimbali vya usafiri ili mradi tu wamekuja kwenye mkutano wa RSA.
Hakika nawapongezeni sana. Mkutano nimeambiwa umeenda kwa utulivu sana, mada ya bima wengi mmeifurahia na kuonesha kuitaka Zaidi. Nadhani mtatupa feedback hapa. Wengi mmekaa hadi mwisho wa mkutano, mmenunua fulana za RSA na ktoa michango mbalimbali ya mawazo kwaajili ya kuboresha RSA. Mimi kama kiongozi ninaona nawiwa deni kubwa kwenu kuendelea kuratibu RSA kutoka popote duniani, na sasa ninaona kuwa juhudi zangu si bure haziishii patupu.Ninawashukuruni sana kwa kutambua michango ya RSA mbalimbali katika kuimarisha RSA kwa kuanzia na admins, mimi mwenyewe hususani, Mwenyekiti, Katibu, Kamati tendaji, RSA mmoja mmoja, Kamati ya zawadi na tuzo nk. Kwa namna ya pekee nazidi kumpongeza na kwa kweli nashindwa niweke neon lipi ili niwape uzito unaostahili, Kamanda Mohammed Mpinga na Johansen Kahatano kwa moyo wao wa dhati wa kuwa tayari kufanya kazi na RSA. Tangu, Mwaka 2014 December, tulipokutana mara ya kwanza kwaajili ya kuwa na mkutano wa kwanza na kuifanya rsa isimame kama taasisi, Mpinga na Kahatano wameendelea kuisapoti RSA kwa hali na mali. Wameendelea kufanya kazi na sisi bega kwa bega, wameendelea kutufadhili kutumia ukumbi wa polisi pamoja na vifaa vingine kufanyia mikutano. Hii sasa ni changamoto kwetu RSA kuweza kujiimarisha ili kujitegemea, tuwe na ofisi zetu hata kama sio ofisi kama ofisi basi uwezo wa kuwa na fedha kwaajili ya kukodi ukumbi wa mikutano, kuendesha mikutano yetu na kampeni zetu mbalimbali. Naamini kwa umoja huu na ushirikiano wetu tutafika na tutayatimiza yote haya.Lengo letu ni kukabiliana na hili jinamizi la ajali kwa kusisitiza utii wa sheria bila shuruti. Shukrani za pekee ziwaendee Adam Phillip-Mwenyekiti wa Kamati ya Muundo wa Kitaasisi na Bw. Justine Mwandu kwa mawasilisho yao ya leo. Kuanzia sasa RSA natangaza kauli mbiu mpya ya RSA. Kauli mbiu yetu mpya ni “USALAMA BARABARANI NI HAKI NA JUKUMU LETU SOTE” Kwa maana ya kwamba kila mtu ana haki ya kuwa salama barabarani na pia ni wajibu kila mmoja wetu kuhakikisha barabarani kunakuwa salama. Hivyo ningependa hata salama yetu iwe “Usalama barabarani”Jibu: “Ni jukumu langu”. Kila mmoja aseme hivi moyoni mwake na kwa kinywa..Pia palikuwa na Semina za Kampuni za Bima;- Leo RSA mtapigwa shule ya maana sana kuhusu bima, ni nafasi yenu kuwahi ili kupata uhondo wa somo la bima toka kwa nguli wa tasnia ya Bima ambaye uzoefu wake wa kinadharia na kivitendo kwa muda mrefu hauna chembe ya shaka kuwa anaifahamu vema tasnia hiyo. Wewe jipange tu na maswali yako, tumempa muda wa saa nzima kufanya wasilisho lake na kujibu maswali. Kwa ufupi tu Mr. Mwandu ni mwalimu(lecturer) na mtendaji (practitioner) ktk tasnia ya masuala ya bima. Amepata kufundisha watu wengi darasani na pia kuwasimamia kama mkuu wa kazi na mkuu wa shirika la bima la taifa. Mr. Mwandu ameshiriki ktk mageuzi ya sekta ya bima nchini Tanzania hivyo ukikosa somo la leo utakuwa umekosa mambo mengi sana. Jongea ukimbini mara moja kwani wakifika watu 20 tu mkutano unaanza.



Pia Mwenyekiti alikumbushia ya kikao cha Mwaka jana December; -MOJA YA ILIYOWAHI KUWA MIJADALA MIREFU SANA YA RSA KUHUSU NOTIFICATION KATI YA JUNE 20-24, 2014SWALI/HOJANaomba kukumbushwa hivi ni kwa nini ikiwa na kosa la barabarani traffic police wanangangana ukifika kosa na ilipe fine hapo barabarani ... Na ukiwaelezea options zilizopo ktk notification wana kuwa wakali, na kusema uache leseni ama gari ....Kama tatizo ni watu kuingia kiti ni basi si notification zibadilishwe ....maana sidhani Kama ni sawa maduhuli ya serekali kukusanywa maporini na wasio hata watu za fedha! Fungo Augustus nisaidie kwenye hili, maana ukigoma kutoa hela ya soda/chai unalazimika kubishia notification na government revenue receipts..... #‎tubadilike•        John Seka Hahaaa. Vile vitabu sio vya ukweli. Wengi wamechongesha!! Ila jibu zuri anaweza kutupa mkuu wa trafiki kamanda Mohammed Mpinga•        Asina A Omari John Seka leo mie nimegombezwa sana baada kusema niandikie nielekeze nikalipie wapi ....na sio Mara ya kwanza ....mie naomba kamanda Mohammed Mpinga anipe trusted status na cheti kuwa nikifanya kosa nitaenda lipia kwa OCD anaye husika ....it feels soo funny kulipia hela barabarani. Leo mie wamenirudishia hela zangu maana niliwaambia hatuachi leseni wala nini na notification iambatane na grr Kama wako busy kukusanya maduhuli porini! Kwa hasira waka nirushia hela zangu na kusema mie sio mlipaji ....alafu hawaja vaa number zao! Yaani hizi tochi naomba nihadithie siku nyingine habari yake ...kamanda hao watu wenu barabarani wanatugeuza mitaji na tochi zao!•        Prudens Rweyongeza Mimi utaratibu wangu siku hizi silipi pesa barabarani and after all si lazima niwe na pesa kwenye wallet! This needs clarification Asina A Omari•        Asina A Omari Si ndo hapo! Pia what if na kataa kosa? Prudens Rweyongeza•        Angelo Rumisha Maana ya kulipia notification maana yake unakubali kosa. Lakini notification siyo lazima ulipa on sport. Kuna sheria na utaratibu wa notification ni mzuri ila changamoto iko kwenye usimamizi wa sheria•        Fungo Augustus Ngoja na mimi niseme. Ni kweli utaratibu wa kulipia faini barabarani kwa askari ilhali askari wenyewe hawana risiti unakera sana. Afande Mohammed Mpinga alishawahi kulikubali hili hapa na kueleza kuwa kwa kawaida ilitakiwa polisi wasipokee kbsa hizo pesa kama ingekuwa uamuzi wake na akasema kuna utaratibu unafanyika kuhakikisha polisi hawapokei hizo hela au wengine wanavyotaka, zitumike efd.•        Fungo Augustus Ile notification ina sehemu mbili moja ya kukubali kosa na kulipa hapo hapo au kulipia kituoni na ya pili ni kukataa kosa hivyo upelekwe mahakamani. Wengi huwa tunaopt kukubali kosa sasa shida inakuja pale tunapotakiwa kulipa kwa wale askari ambao hawana risiti za exchequer unalipishwa tu na kupewa notification. Na hatuna uhakika zile pesa hufikishwa kwa mhasibu au hata km vile vitabu ni halali. Lkn jambo jingine hata ukaamua utalipa kituoni? Askari ataaminije kuwa utacomply hivyo akuachie uende? Ndo maana ukiinsist wengine watataka uache leseni au uliache gari au ukalipaki polisi then ukalipe kisha uje uchukue gari. Hapa ndipo kero kuu ilipo bi Asina A Omari sasa mimi huwa naamua kulipa then nachukua jina na namba ya askari na kituo nikirudi toka safari huwa nafuata risiti yangu.•        Mohammed Mpinga Nipo likizo sikuweza kuuona mjadala huu mapema. Nashukuru kwa maelezo ya Fungo Augustus naona alinielewa vizuri katika maelezo yangu ya nyuma - Ahsante sana. Utaratibu wa Electronic ticketing uko katika mchakato unakuja. Sikatai kunaweza kuwa na notification fake kama ambapo hata GRR inaweza kuwa fake lakini ieleweke notification (PF 101) ni doc ya serikali hivyo iaminiwe katika ulipaji na risiti yako utaipata tu baadae tatizo madereva wengi wanakubali makosa lakini wanaweka kisingizio cha kutaka risiti ili wasilipe faini. Mabishano yanakuwa makubwa na kuchukua muda, 'kwanza ni fake mbona ya 2011, speed sio yangu, alama iko wapi, mbona mko polini, rushwa tu, mnanionea, hamnijui mimi, nampigia .... utakoma n.k.' YOTE hii hupelekea baadhi ya askari kuamua kuwaachia. Kwa kweli ni usumbufu usio wa lazima na ndio matunda ya kuto tii sheria - kuepuka yote haya tuzingatie UTII WA SHERIA BILA SHURUTI.•       
Asina A Omari Asante kwa maelezo Fungo Augustus nadhani maelezo yako ni vema sie madereva wote tukayaelewa. Ila reservation yangu ni moja tu kwamba utaratibu huu unassume nimetembea na hela ....pia unassume kuwa mie naenda kukaa mahali maana na weza kuwa naenda naminywili kusalimia narudi same day sasa naambiwa nirudie receipt kesho why? Najua kuwa wengi wetu tutaingia mtini tukiwa na utaratibu wa kistaarabu wa Kutii sheria bila shurti na kuaminiana ....so hizo electronic ticketing/citations mie nazingojea kwa hamu sana! Kamanda Mohammed Mpinga tatizo sie raia wengi tunaanza kubembeleza na kujijengea wenyewe mazingira ya kuombwa hela ya chai ...Mara nyingi askari ana kuwa ana reciprocate tu nia ya raia ya kusuggest atoe kitu kidogo asemehewe. Sasa sie ambao hatujawahi master the art ya kubembeleza Askari barabarani ukikutana na Askari ananza kuona unamdharau kisa baada ya kujua kosa umesema niandikie, kumbe we una taka tu umalize uendelee na shughuli zako. Habari ya kupiga simu kwa mtu kisa umekamatwa na traffic ni TABIA MBAYA (unless kuna shida nyingine zaidi ya kosa ulio fanya). Ila pia kamanda wasihi Askari wasitubambikie makosa ya ku overspeeed maana haiwezekani gari kadhaa zote zina enda speed hio hio sehemu hio hio imepimwa na mtu huyo huyo ....probability na margin of error hapo inakuwaje!?•        Janemary Ruhundwa Nami nikushukuru Kamanda Mohammed Mpinga kwa kutukumbusha utaratibu. Nakubaliana na wewe kuwa ni muhimu kuacha leseni endapo umekutwa na kosa na hauna uwezo wa kulipa on the spot ili watu wasiingie mitini. Tatizo nililokutana nalo mimi mara kadhaa ni kuwa ninapossugest niache leseni Askari wanakataa na wanadai nikaache gari kituoni hadi nitakapopata pesa ya kulipa fine. Na maelezo ni yale yale kuwa naweza kuingia mitini nisirudi kuchukua leseni yangu.•        Janemary Ruhundwa Kwa ufahamu wangu ni kuwa hizi leseni mpya zina information zote za muhimu zinazonihusu na endapo nitadefault kuna mengi tu yanaweza kufanywa kunilazimisha nikalipe hiyo fine. Kwanza kuna namba yangu ya simu kwenye system, pili hii leseni ipo linked na TIN yangu so TRA wanaweza kuwa notified kuwa nimedefault nikakamatwa wakati wa kulipia Motor Vehicle licence nk. sasa nashindwa kuelewa kwa nini leseni isiwe dhamana tosha endapo nashindwa kulipa on the spot. Na ninachoshangaa zaidi ni kwamba Kamanda Mpinga ulituambia kuhusu hii option ila Askari wako huko njiani hawana taarifa nayo kabisa, hasa hawa wa barabarani za mijini. Elfu 30 si ndogo na si kila mtu anatemea nayo kila wakati. naamini ndio maana hata notification imetoa option ya kulipa fine within some days.•        Janemary Ruhundwa Na pia naungana na Asina kuwa kuna makosa ni ya kubambika kabisa hadi unashangaa. So si kuwa watu hatutaki kutii sheria kuna muda makosa yanaibuliwa hata unashangaa yametokea wapi.•        Asina A Omari Janemary Ruhundwa umenikumbusha Siku nimekamatwa na askari ananiuliza kwanini gari yako chafu sana ...... Alafu ni saa mbili asubuhi Siku ya jumapili ....yaani Nilishiwa nguvu ...! Mie nadhani the best method ni kuharakisha e-ticketing maana kuacha leseni mbwewe wakati naenda Arusha nayo ni issue! Ndio notification nitakuwa nayo but jamani wengine leseni wanatumia Kama ndio Kitambolisho! Technolojia ya e ticket wala sio ngumu jamani na leseni zina bar code ....mie nasikitikia mapato ambayo serekali inakosa toka kwa wanao amua kubembeleza kuliko kulipia fine maana logistics za fine ni usumbufu!•        Mohammed Mpinga Janemary Ruhundwa ni kweli CDL zetu zina information nyingi sasa tukisuburi mpaka utakapokwenda kulipa MV licence miezi 10 ijayo ndipo ulipe faini yetu sijui itakuwaje. Hata hivyo utaratibu wa anuani utatusaidia baadae kuwekewa bill yako nyumbani kwako. Ni kweli kuna baadhi ya madereva wanaacha leseni zao Polisi, ni kwamba askari anapochukua leseni au kubaki kituoni, dereva huyo huenda mkoa mwingine anaripoti Polisi amepoteza au kuibiwa na anapokwenda TRA anapata nyingine ! kwa hiyo harudi tena Polisi kulipa faini na leseni inabaki kituoni (bado hatuna utaratibu mzuri wa kufuatilia kwa wanao pata leseni baada ya kupotea au kuibiwa) - zipo leseni nyingi kwa sasa vituoni zilizoachwa na madereva hawatokei kuzichukua.•        Janemary Ruhundwa Duuh hao watu wana mahesabu mahali kweli. Fine ya elfu thelathini ukimbie ukaanze process ya kuomba leseni mkoa mwingine kisha uilipie 40,000! Labda kama wana fine kubwa. Na pengine kuna haja ya kutofautisha hapo, kiwango cha fine, probability ya mtu kutorudi (mnaweza kuangalia masuala kama yale mnayoangalia wakati wa kuwapa watu dhamana, ukiondoa habari za utambulisho Wa serikali za mitaa of course). Yaani akili yangu inagoma kuamini na kuelewa kuwa mbadala Wa kulipa fine ya Tshs 30,000 ni kuacha gari kituoni. Hata hizo e ticket zikianza bado kuna issue ya mtu kuwa na hela hapo hapo anapokamatwa.•      
Asina A Omari ,Janemary Ruhundwa umeona ambavyo tunatofautiana akili ….maana usumbufu wa kutafuta leseni mpya khaaa!!! anyhow mie nilisha sikia mahali mtu analipa rushwa 20m ili asidaiwe deni la 35m badala ya kupunguza deni! hilo la kuwa na hela hapo hapo nalo ni tatizo ndio maana mie am all for niambiwe nikalipe wapi na nisipo lipia nikutane nayo TRA …mbona kwa nchi nyingine ndio hivyo tunaishi ….utakimbia deni weeee ipo siku unakutana nalo na penalty juu!!! hii italeta efficiency katika ukusanyaji lakini pia katika mapato kutoingia mifukoni mwa watu! Ifike mahali tuwe responsible citizens kwa kutii sheria bila shurti, ila na mamlaka nazo zitusaidie kutii sheria.•        Janemary Ruhundwa Ha ha haaa, hizo ndio zinaitwa akili matope. Mie nakubaliana na wewe, tukalipe mahali maalum, na tupewe muda wa kulipa kama hatuwezi kulipa siku hiyo hiyo. Penalty ya kudefault iwe kubwa period. Mbona motor vehicle tunalipia na tupo makini sana maana tunajua tukivusha mwezi penalty ni 100% Tatizo la defaulters haliwezi kuisha ila nadhani we have to choose a lesser evil.•        Fungo Augustus Nadhani kwa mjadala huu na mingine mipana ijayo inaweza kuboresha huu utaratibu wa kulipa faini, mfano uholanzi fine ni kama mara tatu ya malipo halali kwa baadhi ya makosa. Mf. Bima, Parking and Crossing Zebra or Red Lights without stopping na hakuna uniform penalty km hapa bongo. Sijajua kwa nini kila kosa fine yake ni 30,000 Mohammed Mpinga maana makosa mengine ni madogo mno au ya onyo tu wakati mengine ni makubwa sana kutozwa elfu 30. Hili lifanyiwe kazi.
Afu pia uzoefu wangu unainesha kuwa askari ukishampa leseni yako lazima atafute namna ya kuiretain kwa kukutafutia kosa ila usipompa ni rahisi kukuachia so mara nyingi huwa nadeclare kusahau leseni au kutoa copy japo kwa sasa kwakuwa nishajua kuwa askari atakayetaka kubaki na leseni yangu itabidi anijazie form no 114 hili ndo ntalitumia zaidi•       
Asina A Omari Fungo Augustus umenikumbusha kitu hio PF 114 ni muhimu sana maana hii biashara ya kubadilishana number za simu na askari sio rasmi after all ile ni simu yake binafsi anaweza akaamua kuzima au akapata amri ya kuondoka alipo sasa leseni inakuwaje?? Janemary Ruhundwa ni kweli akili ni nywele! defaulters watakuwepo hio ndo fact but sie wengine tusiteswe kisa kuna wachache watakao default! I hope haya yote ytunayo toa kama mawazo yataat least kufikiriwa maana ….•        Mohammed Mpinga Nimesoma mawazo ya wengi kwa hakika ni mazuri tutayafikisha kwa wadau wenzetu na kama yatakubalika mwisho wa siku. Aidha kule SA J'Burg ukipatikana na Traffic Offence ukilipa pale pale unapata punguzo lakini kadri siku zinavyoongezeka kwa kosa hilo hilo utalipa zaidi na pia makosa hayalingani kwa faini tofauti na kwetu ambapo kosa lolote mmoja ni Tshs 30,000, pia wana mfumo mzuri wa kufuatilia wasiolipa fine.•       
John Seka Jamani hivi kungekuwa na askari 20 wenye akili kama kamanda Mohammed Mpinga nchi hii ingefika mbali sana. Ukiacha askari ambao ni classmates wangu sidhani kama nishawahi kukutana na askari engaging na anayejua polisi jamii. Sidhani kama ntakuwa nakosea kumtabiria makubwa Kamanda Mpinga (ingawa ofkoz wale wenzake wanaweza kuhisi anatafuta umaarufu) #mawazonandoto# Asina A Omari Janemary Ruhundwa Augustus FungoKamanda Mohammed Mpinga na Afande Johansen Kahatano wana kile kinachoitwa responsible leadership jambo ambalo kwa wenye akili finyu au akilisiasa watasema wanatafuta umaarufu ila kwa kweli kwa mtu km Mpinga kwa nafasi aliyonayo angeweza kujitetea sana kwamba hatujibu coz is too busy but muda mchache alionao anatufaidisha sana hapa na kikubwa yuko tayari kukiri udhaifu na kupokea mawazo mapya.
Emmanuel Kihaule hawa wawili Mohammed Mpinga na Johansen Kahatano ni Exceptional Kwa kweli kikao kilihudhuriwa na wajumbe kutokea mikoa mbalimbali Tanzania'walio mikoani walipata muendelezo wa kikao kupitia mitandao ya Kijamii km Telegram kwenye RSA-KULIKONI BARABARANI yenye wajumbe zaidi 150 hivi pia WhatsApp ya  RSA-KULIKONI BARABARANI-MKOA KILIMANJARO;
Pia Kamanda Mohamed Mpinga aliwapongeza japo yuko likizo:- Hongereni kwa kikao, naona kinakwenda vizuri, ahsanteni kwa clips mlizotuma.Pole sana Gagedu naamini bila shaka ulivaa Helmet na kama hukuvaa fikiria ingekuwaje, pia alitoa pole kwa mjumbe aliyepata ajali ya Pikipiki..
Kikao kiliendelea huku Mlezi wa RSA-anakaimu nafasi ya Kamanda Mohamed Mpinga alikuwepo Afande Kahatano ndiye alikuwa kwa niaba ya Kamanda hakika maswala yalikwenda Vizuri sanaaa!!!

Na Kauli mbiu;-USALAMA BARABARANI, NI JUKUMU LETU SOTE!!Wenu;

Mtanzani Jitambue-Dar es Salaam 29/03/2015

0 maoni:

Chapisha Maoni

Inaendeshwa na Blogger.

Machapisho Maarufu

Machapisho ya Karibuni

Recent Posts Widget